MAOFISA wa Uhamiaji wamemnyang’anya Hati ya Kusafiria (passport) Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti isiyo ya kiserikali Twaweza Aidan Eyekuze. Anaandika Regina Kelvin … (endelea).
Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo katika ukurasa wake wa twitter ameandika kuwa ‘baada ya wiki kadhaa taasisi hiyo kuchapisha utafiti wake na matokeo kuonesha umaarufu wa rais kushuka. Hati ya kusafiria ya Eyekuze imekuckuliwa na uhamiaji.’
Julai 6, Twaweza ilieleza utafiti wake kwamba, Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli umeshuka kutoka asilimia 96 mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 55 mwaka huu.
Na kwamba, asilimia 55 ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais Magufuli tangu alipoingia madarakani mwaka 2015. Kukubalika huko kulipungua kutoka asilimia 96 mwaka 2016, na 71 mwaka 2017.
Kiwango cha kukubalika kwa Rais kimeshuka kutoka kwenye rekodi ya juu kuwahi kuwekwa na Rais wa Tanzania mpaka rekodi ya chini tangu takwimu hizi zianze kukusanywa mwaka 2001.
Leave a comment