Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mkurugenzi Twaweza anyang’anywa ‘Passport’
Habari za SiasaTangulizi

Mkurugenzi Twaweza anyang’anywa ‘Passport’

Aidan Eyekuze, Mkurugenzi Twaweza
Spread the love

MAOFISA wa Uhamiaji wamemnyang’anya Hati ya Kusafiria (passport) Mkurugenzi wa taasisi ya utafiti isiyo ya kiserikali Twaweza Aidan Eyekuze. Anaandika Regina Kelvin … (endelea).

Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo katika ukurasa wake wa twitter ameandika kuwa ‘baada ya wiki kadhaa taasisi hiyo kuchapisha utafiti wake na matokeo kuonesha umaarufu wa rais kushuka. Hati ya kusafiria ya Eyekuze imekuckuliwa na uhamiaji.’

Julai 6, Twaweza ilieleza utafiti wake kwamba, Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli umeshuka kutoka asilimia 96 mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 55 mwaka huu.

Na kwamba, asilimia 55 ya wananchi wanaukubali utendaji wa Rais Magufuli tangu alipoingia madarakani mwaka 2015. Kukubalika huko kulipungua kutoka asilimia 96 mwaka 2016, na 71 mwaka 2017.

Kiwango cha kukubalika kwa Rais kimeshuka kutoka kwenye rekodi ya juu kuwahi kuwekwa na Rais wa Tanzania mpaka rekodi ya chini tangu takwimu hizi zianze kukusanywa mwaka 2001.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

Regina Mkonde: CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!