Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Mkude, Morrison nje mechi mbili
Michezo

Mkude, Morrison nje mechi mbili

Jonas Mkude
Spread the love

KIUNGO wa Simba, Jonas Mkude na nyota wa Yanga, Bernard Morrison wamefungiwa kucheza michezo miwili pamoja na faini ya Sh. 500,000 kwa makosa ya utovu wa nidhamu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Maamuzi hayo yametoka chini ya Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), chini ya Mwenyekiti wake, Peter Hella ambaye alisoma maamuzi hayo.

Mkude amefungiwa mara baada ya kumpiga kiwiko mchezaji wa timu ya Biashara ya Mara, kwenye mchezo wa Ligi Kuu iliyochezwa tarehe 22 Februari, 2020 kwenye Uwanja wa Taifa.

Bernard Morrison

Morrison aliingia kwenye adhabu hiyo baada ya kumpiga kiwiko mchezaji wa Tanzania Prisons kutoka Mbeya na adhabu hizo zitaanza mara moja.

Klabu hizo zitaanza kuwakosa wachezaji hao kwenye michezo ya leo ya Ligi Kuu, ambapo Simba itashuka dimbani kuikabili Mbeya City, huku Yanga watakuwa Uwanja wa Taifa, kuikaribisha Namungo FC kutoka Lindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!