Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Milioni moja wafariki dunia kwa corona
Habari

Milioni moja wafariki dunia kwa corona

Spread the love

WAGONJWA milioni moja duniani wamefariki kutokana na virusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Mtandao wa worldometer umeripoti leo Jumanne tarehe 29 Septemba 2020, waliopona kutokana na ugonjwa huo ni milioni 24.89 huku maambukizo yakifikia milioni 33.57.

Marekani imeendelea kuwa Taifa linaloongoza kwa maambukizo milioni 7.36, kati yao waliofariki dunia wakiwa 209,808 na waliopona virusi hivyo ni milioni 4.6.

India inafuatia ikiwa na maambukizo milioni 6.14, waliopona milioni 5.1 na waliofariki dunia 96,351. Brazil inashika nafasi ya tatu ikiwa na maambukizo milioni 4.74, waliofariki 142,161 na waliopona ugonjwa huo wakiwa milioni 4.

China ambako corona ilianzia mwishoni mwa mwaka 2019 ina maambukizo 85,384 na vifo vikiwa 4,634 na waliopona wakiwa 80,566

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!