Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Taratibu za kimila zatumika kutafuta wauaji
Habari Mchanganyiko

Taratibu za kimila zatumika kutafuta wauaji

Maelfu ya wakati wa Karatu wakiwa katika mazishi ya Afisa Elimu Maalum wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu, Martin Goi (picha ndogo)
Spread the love

MAELFU ya wananchi wameshiriki katika mazishi ya Afisa Elimu Maalum wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu, Martin Goi, aliyeuawa kwa kupigwa risasi na wanaoitwa na serikali, “watu wasiojulikana.” Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Goi alipigwa risasi tarehe 15 Januari mwaka huu, katika mgahawa wa Rhotian Glades, wilayani Karatu, majira ya saa tatu usiku. Goi alizaliwa katika kijiji cha Dofa wilayani Karatu.

Taarifa zinasema, mara baada ya shambulio hilo na kabla mauti kumfika, Goi alipelekwa kwenye hospitali ya Sanawati mkoani Arusha. Alifia katika hospitali hiyo siku mbili baada ya kushambuliwa.

Kwa mujibu wa habari hizo, mara baada ya marehemu Goi kuzikwa, wananchi kadhaa walishiriki katika maombi maalum ya kumtambua waliofanya mauaji hayo.

Maombi hayo yalihitimishwa jana tarehe 22 Januari kwa dua na sala za kimila na kidini. Kwa kawaida, maombi ya aina hiyo hujibu katika kipindi kifupi cha wiki moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!