Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mil 180 zachangwa leo kusaidia waathirika ajali MV Nyerere
Habari MchanganyikoTangulizi

Mil 180 zachangwa leo kusaidia waathirika ajali MV Nyerere

Spread the love

MPAKA kufikia saa 12:00 jioni ya leo tarehe 23 Septemba 2018, jumla ya Sh. Mil 180 zimechangwa kwa ajili ya kusaidia walioathirika kwenye ajali ya MV. Nyerere. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Wadau waliotoa michango hiyo mpaka sasa ni Vodacom (Mil 10), Tigo (Mil 150), Azim Dewji (Mil 10) na Waislam jamii ya Shia (Mil 10).

Pia michango mingine imeendelea kutolewa ikiwa ni pamoja na katoni za maji zaidi ya 6,000.

Serikali leo imefungua akaunti maalum kwa ajili ya kuchangia waathirika hao. Akaunti hiyo ni ‘Maafa ya MV Nyerere 31110057246 Tawi la MNB Kenyatta, Mwanza.’

Wadau hao wametoa michango hiyo leo katika Kisiwa cha Ukara ambapo ajali hiyo ilitokea Septemba 20, Mwaka huu.

Jenister Muhagama, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu akizungumza katika Kisiwa cha Ukara amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella kuhakikisha fedha hizo zinatumika kwa waathirika.

Amesema, ofisi yake itakuwa inaikagua akaunti hiyo mara kwa mara ili kuhakikisha malengo mahususi yanafikiwa.

Na kwamba, akaunti hiyo itasimamiwa na kuratibiwa na kitengo cha maafa cha Mkoa wa Mwanza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!