JABIR Idrissa, aliyekuwa Mhariri wa Gazeti la MwanaHALISI, ameshinda kura za maoni za ubunge kupitia Chama cha ACT-Wazalendo katika Jimbo la Pangawe, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Unguja … (endelea).
Jabir aliyekuwa mmoja wa waajiriwa wa Kampuni ya Hali Halisi Publishers Ltd (HHPL), iliyokuwa ikizalisha magazeti ya MwanaHALISI, Mseto na Mawio amepata kura 41 dhidi ya mpinzani wake Hamad Ali Hamad aliyepata kura 36. Bahamadi alikuwa mbunge wa Magogoni, mjini Zanzibar mwaka 2010-2015.
Washindani wengine kwenye kura hizo walikuwa Aminie Mohamed Juma aliyepata kura 20 na Juma Khelef Juma aliyepata kura tano kati ya kura 103, kura moja iliharibika.
Jabir alianza kuitumikia Kampuni ya HHPL mwaka 2006 akitokea gazeti la Mtanzania.
Magazeti la MwanaHALISI, Mseto na MAWIO yamefungwa na serikali kwa kudaiwa kufanya uchochezi. Jabir alijiunga na chama hicho visiwani Zanzibar mwaka jana.
Leave a comment