Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mhariri MwanaHALISI apenya kura za maoni Z’bar
Habari za Siasa

Mhariri MwanaHALISI apenya kura za maoni Z’bar

Jabir Idrissa
Spread the love

JABIR Idrissa, aliyekuwa Mhariri wa Gazeti la MwanaHALISI, ameshinda kura za maoni za ubunge kupitia Chama cha ACT-Wazalendo katika Jimbo la Pangawe, Wilaya ya Magharibi B, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Unguja … (endelea).

Jabir aliyekuwa mmoja wa waajiriwa wa Kampuni ya Hali Halisi Publishers Ltd (HHPL), iliyokuwa ikizalisha magazeti ya MwanaHALISI, Mseto na Mawio amepata kura 41 dhidi ya mpinzani wake Hamad Ali Hamad aliyepata kura 36. Bahamadi alikuwa mbunge wa Magogoni, mjini Zanzibar mwaka 2010-2015.

Washindani wengine kwenye kura hizo walikuwa Aminie Mohamed Juma aliyepata kura 20 na Juma Khelef Juma aliyepata kura tano kati ya kura 103, kura moja iliharibika.

Jabir alianza kuitumikia Kampuni ya HHPL mwaka 2006 akitokea gazeti la Mtanzania.

Magazeti la MwanaHALISI, Mseto na MAWIO yamefungwa na serikali kwa kudaiwa kufanya uchochezi. Jabir alijiunga na chama hicho visiwani Zanzibar mwaka jana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!