Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mhagama akumbusha uzalendo watumishi wa Mashirika ya Kimataifa
Habari za Siasa

Mhagama akumbusha uzalendo watumishi wa Mashirika ya Kimataifa

Jenista Mhagama, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu)
Spread the love

JENISTA Mhagama, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu) ametoa wito kwa Watanzania wanaofanya kazi katika Mashirika ya Kimataifa kuitumia fursa hiyo katika kusukuma gurudumu la maendeleo ya taifa lao. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mhagama ametoa wito huo leo tarehe 15 Juni 2019 wakati akizungumza katika Kongamano la Nne la Tafa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lililofanyika Jijini Dodoma.

Akitolea mfano wa Amon Manyama, Mkuu wa Programu wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP), Mhagama amesema ni vyema Watanzania hao wakaiga mfano wake katika kutumia mashirika yao kuchochea ustawi wa Watanzania.

“Tunayo mashirika mbalimbali ya kimataifa yanayofanyakazi ndani ya taifa letu, na Watanzania wamepata fursa ya kutumikia mataifa hayo. Lakini kazi anayofanya Manyama kama muwakilishi kwa ustawi wa Watanzania ni kubwa sana,” amesema Mhagama na kuongeza:

“Labda tu nichomekee hapo, Watanzania wengine ambao wako katika mashirika mbalimbali ya kimataifa watusaidie kama kazi anayofanya ndugu yangu Manyama. Sisemi kama hawafanyi ila watufikishe kama anavyofanya Manyama.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!