TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), haijamteua David Mwaijojele wa Chama Cha Kijamii (CCK) kuwa mgombea urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020 baada ya kushindwa kukidhi masharti yaliyowekwa kwa mujibu wa Katiba na sharea. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea)
Mwaijojele ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho, ameshindwa kuteuliwa leo Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage baada ya kuwasili ofisi za tume hiyo jijini Dodoma akiwa peke yake.
Katibu wa NEC, Dk. Willson Mahera amesema, baadhi ya masharti aliyoshindwa kukidhi ni kutokujazwa fomu namba 10 ya mgombea mwenza na picha za mgombea mwenza.
Kwa upande wake, Mweneykiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage amesema tume hiyo imeshindwa kumteua David Mwaijojele kuwa mgombea wa urais baada ya kutokukidhi masharti ya Katiba na sheria za uchaguzi.
Mwaijojele amekuwa mgombea wa kwanza kati ya 17 kutokuteuliwa kugombea nafasi ya juu ya uongoza wa Tanzania kati ya wagombea 12 waliorejesha na kuteuliwa.
Tofauti na vyama vingine 12, Mwaijojele amewasili ukumbini akiwa peke yake tofauti na wagombea wengine waliowasili akiwa na viongozi na wanachama wa vyama hivyo.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali
Leave a comment