Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mgogoro wa miaka 40 wapatiwa ufumbuzi
Habari Mchanganyiko

Mgogoro wa miaka 40 wapatiwa ufumbuzi

Aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula
Spread the love

MGOGORO uliodumu kwa zaidi ya miaka 40 kati ya jeshi la Polisi na Wananchi wa mitaa miwili ya Songambele na Kigoto mkoani Mwanza ambao wanadaiwa kuvamia eneo hilo, sasa umepatiwa ufumbuzi wake. Anaripoti Moses Mseti, Mwanza … (endelea)

Eneo hilo lenye ukubwa wa hekari 41, Wananchi hao wanadaiwa walivamia eneo hilo lenye kaya 461na kujimilikisha eneo lililokuwa mali ya jeshi la Polisi.
Akizingumza katika eneo hilo la Kigoto kwa niaba ya Rais DK. John Magufuli, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumban na Maendeleo ya makazi Angelina Mabula, alisema kuanza sasa ( Jana )wananchi wote wanaoishi eneo hilo ni wakazi halali.
Alisema lengo la serikali ya awamu ya tano ni kuwatetea wananchi wanyonge, hivyo serikali imeamua wananchi hao kuendelea kuishi eneo hilo.
“Wananchi ambao wanaishi hapa waendelee kama kawaida lakini lile eneo la hekari 17 ambalo halijavamiwa lisiguswe na mtu, pia jeshi la Polisi tutawatafutia eneo lingine.
“Wananchi mnaoishi hapa kuanzia sasa maeneo haya lazima yalasimishwe rasmi ili muweze kuyamiliki kihalali na mpate hati zenu,” alisema Mabula.
Mabula ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilemela, pia alitaka wananchi hao kulipa  gharama endelea sahahi za umilikishwaji maeneo hayo ambazo zimewekwa na serikali.
Alisema wananchi hao awali walikuwa hawafahamu hatima yao juu ya makazi yao kama yatachukuliwa na jeshi hilo ama vinginevyo, ambapo amedai kuwa hatma ya imepatikana baada ya rais (John Magufuli) kupata taarifa za mgogoro huo na kuchukua aliamua hatua.
Akizungumza baada ya kikao hicho, mmoja wa wananchi hao, Elizabeth Charles alisema maeneo hayo zamani walikuwa wanauziwa na watu na kwamba wait walikuwa hawafahamu kama ni mali ya jeshi la Polisi hivyo waliendelea kuishi eneo hilo kwa muda mrefu.
“Tunamshukuru rais John Magufuli kwa uamuzi wake wa kutusaidia sisi wanyonge kuendelea kuishi eneo hili, sisi hatuna cha kumlipa zaidi ya kumshukru na ukiangalia makosa sio ya kwetu ni ya wale ambao walikuwa wanatuuzia,” alisema Elizabeth.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!