Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mgogoro wa ardhi waibuka upya Karagwe
Habari Mchanganyiko

Mgogoro wa ardhi waibuka upya Karagwe

William Lukuvi, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Spread the love

MAMIA ya wananchi wa kijiji cha Chabuhora, wilayani Karagwe, mkoani Kagera, wanahitaji msaada wa haraka wa chakula, baada ya mashamba na nyumba zao kuchomwa moto katika kinachoitwa, “operesheni maalum ya mkuu wa wilaya hiyo, anaandika Joseph Sekiku.

Taarifa kutoka Karagwe zinasema, mkuu huyo wa wilaya aliamua kuchomwa moto nyumba na  mashamba hayo ya wananchi, kwa madai ya kutaka kuwabeba wafugaji.

Taarifa zinasema, wananchi wanaoishi katika maeneo hayo, wamekuwapo kwa miaka kadhaa sasa; wanamiliki maeneo hayo kwa kibari cha serikali ya kijiji.

“Lakini mkuu wa wilaya amefika hapa. Ameanza kuchoma moto nyumba za wananchi na kuwahamisha kwa nguvu.

Anadai sisi ni wavamizi, wakati tumemilikishwa maeneo hayo na serikali za kijiji na tumekuwapo hapa tangu enzi na enzi,” ameeleza mzee mmoja wa makamo kwa sharti la kutotajwa jina.

Anasema, serikali  wilayani humo imekuwa ikidai kuwa wananchi hao wameondolewa katika maeneo hayo kutokana na kuvamia vyanzo vya maji.
Anasema, “serikali ya kijiji imetoa ardhi kwa kaya zile ili waishi na walime.

Hata stakabadhi wanazo. Lakini sasa wameondolewa katika eneo hilo na kuwacha wapweke. Mvua za masika zimeanza na wananchi hawa hawana pa kulala na hawana chakula.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!