NYUMBA ya Tryphone Jeremiah, mkazi wa kijiji Kijiji cha Kishanda B, kilichopo kwenye Kata ya Kibale, Kyerwa mkoani Kagera imechomwa moto. Anaandika Mwandishi Wetu…(endelea).
Pia wanyama wake wameuawa pamoja na migomba, mikahawa yake kukatwakatwa. Waliofanya tukio hilo ni wanakijiji wenzake kutokana na mgogoro wa ardhi.
Taarifa zaidi kutoka kijijini humo zinaeleza, wanakijiji hao zaidi ya 250 walifanya tukio hilo Jumapili wiki iliyopita.
“Wanalalamika kwamba namiliki ardhi kubwa,” amesema Jeremiah akieleza mgogoro wake na wanakijiji wenzake “wamevamia shamba na kufyeka mazao zaidi ya hekta 10.5, wameua mbuzi wangu na kuwachoma moto.”
Amesema, mgogoro wake na wananchi ulianza mwaka 2007 kwa baba yake ambaye alilalamikiwa kumiliki ardhi hiyo. Wakati wanakijiji hao wakifanya uharibifu huo, wachungaji walikimbia kukwepa kuuawa.
Ahmed Msengi, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera ameeleza, mazao ya kahawa, migomba na miti vimeharibiwa vinaya na wananchi hao.
Medius Atanas, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kishanda B amesema, wanakijiji wamekuwa wakilalamikia Jeremiah kumilikisha ardhi kubwa.
Amesema, wanalalamika kumiliki ardhi ambayo si yake hivyo aliamua kufanya vurugu kwa kuchoma nyumba yake, kuua mifugo jambo ambalo halikubaliki.
Leave a comment