Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Tangulizi Mfungwa mmoja kutumia laki moja kwa siku
Tangulizi

Mfungwa mmoja kutumia laki moja kwa siku

Spread the love

WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi imesema gharama za chakula kwa mfungwa mmoja kwa siku ni wastani wa shilingi 1,342. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Hayo yalielezwa leo bungeni na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamadi Masauni alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Njombe Mjini, Edward Mwalongo (CCM).

Katika swali hilo Mwalongo alitaka kujua Serikali inatumia kiasi cha shilingi ngapi kuhudumia mfungwa mmoja kwa siku kwa ajili ya chakula.

 “Vitendo kama kulala chini, kulala bila blanketi au shuka vimekuwa vya kawaida kabisa katika Magereza yetu. Je hii nayo ni sehemu ya adhabu ambayo wafungwa wanapewa kwa mujibu wa sheria,” alihoji Mbunge huyo.

Akijibu, Masauni amesema Jeshi la Magereza katika kutekeleza majukumu yake pia hutoa huduma ya chakula kwa wahalifu kupitia bajeti iliyotengwa na Serikali kila mwaka wa fedha.

Naibu Waziri huyo amesema gharama za chakula kwa mfungwa mmoja kwa siku ni wastani wa shilingi 1,342.

Amesema Serikali imeendelea kuboresha huduma za wafungwa na mahabusu kwa kununua vifaa mbalimbali vya malazi ikiwemo, magodoro shuka, mablanketi na madawa ya kuua wadudu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!