Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mfumo wa JPM wautibua ACT-Wazalendo
Habari za SiasaTangulizi

Mfumo wa JPM wautibua ACT-Wazalendo

John Magufuli, Rais wa Tanzania akihutubia katika sherehe za miaka 55 ya Uhuru
Spread the love

KAMATI ya Uongozi ya chama cha ACT-Wazalendo imeonesha kutofurahishwa na namna ya teuzi za John Magufuli, Rais wa Tanzania zinavyofanyika bila mashauriano na wahusika katika vyama, Jambo hilo limepekea Kamati hiyo kumtaka Rais kuweka mfumo bora wa kuazima watu kutoka vyama vingine, anaandika Hamisi Mguta.

Samson Mwigamba, Kaimu Kiongozi wa chama hicho leo ameyasema hayo wakati akitoa maamuzi ya kikao cha Kamati hiyo juu ya uenyekiti ndani ya chama ikiwa ni siku chache baada ya rais kumteua na kumuapisha Anna Mghwira, Mwenyekiti wa chama hicho kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro bila ya kufanya mashauriano na viongozi wa chama.

“Ili kusimamia maendeleo ya nchi ni vyema kufanya mashauriano na vyama husika ili kuepusha migongano isiyo ya lazima ndani ya vyama na jamii,”amesema Mwigamba.

Aidha, amesema kuwa kutokana na mashauriano ndani ya chama, Mghwira amekoma kuwa Mwenyekiti wa chama na kumteua Yeremia Maganja kuwa Kaimu Mwenyekiti wa chama hadi uchaguzi utakapoitishwa mwezi Machi 2018 hivyo Mghwira atabaki kuwa mwanachama huku akiendelea kutumikia nafasi mpya ya Mkuu wa Mkoa.

Yeremia Kulwa Maganja, aliyekaimu nafasi ya Anna Mghwira

Mwigamba amesema, uteuzi huo wa pili kufanywa na Rais Magufuli katika chama hicho baada ya mwanzoni kumteua Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji ni kielelezo kuwa chama kina watu makini na wanaofaa kuongoza.

Tazama Video hapo chini mwanzo mwisho

Julius Mtatiro, Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi CUF aliwahi kusema kuwa uteuzi wa wa Mghwira haukupaswa kufanywa bila mashauriano kwakuwa viongozi wa chama kimoja kuteuliwa kujiunga na serikali ya chama kingine hufanywa kwa heshima kubwa.

“Kwa kawaida, Rais alipaswa kuwasiliana na Kiongozi Mkuu wa chama na kumjulisha nia hiyo, hata kama Kiongozi Mkuu wa ACT na chama chake wangelikataa, Rais angelikuwa ametimiza wajibu wake wa Ustaarabu wa Kidemokrasia.

“Ndiyo maana, Katibu Mkuu wa UN alipotaka kumteua Dk. Rose Migiro kuwa Naibu Katibu Mkuu wa UN kwanza aliomba ruhusa kwa Rais Kikwete (Rais aw Tanzania), huo ndiyo utaratibu ikiwa uteuzi unafanywa kwa nia njema,” alisema Mtatiro.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!