Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mfanyabiashara wa mafuta kizimbani Manyara
Habari Mchanganyiko

Mfanyabiashara wa mafuta kizimbani Manyara

Spread the love

SIMONI Lemeya Tukai, mfanyabiashara wa mafuta mkoani Manyara na wenzake watatu, wanatuhumiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Manyara … (endelea).

Hivyo, wanatarajiwa kufikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Simanjiro mkoani humo. Watuhumiwa wengine katika sakata hilo ni Ezekiel Fabian Mayumba, aliyekuwa Afisa Afya na Mratibu wa Chanjo ya Mama na Mtoto katika Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro; Ally Sadick Mnkeni na Simaloi Baby Lemeya.

Kwa mujibu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Manyara, Tukai ambaye ni mmiliki wa Kituo cha Mafuta cha Simon Lemeya pamoja na wenzake, watafikishwa katika mahakama hiyo baadaye leo tarehe 22 Juni 2020.

Katika taarifa yao iliyotolewa leo na Holle Makungu, Mkuu wa TAKUKURU mkoani Manyara, watuhumiwa hao wanadaiwa kughushi nyaraka na kufanya ubadhirifu wa fedha za Chanjo ya Kitaifa ya Rubella na Surua na kuisababishia serikali hasara ya Sh. 5.6 milioni.

Taarifa hiyo ya Makungu imeeleza kuwa, watuhumiwa hao wanafikishwa mahakamani baada ya TAKUKURU kufanya uchunguzi na kubaini kwamba, mwaka 2014 walighushi saini za madereva wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro ili kupata fedha hizo.

Tukai na wenzake wanakabiliwa na makosa ya matumizi ya nyaraka kudanganya mwajiri na ubadhirifu chini ya vifungu 22 na 28 vya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2017.

Makosa mengine ni kughushi na kusababishia hasara Serikali kiasi cha Sh. 5,609,00, kinyume cha Sheria ya Uhujumu Uchumi.

“ Ezekiel Fabian Mayumba aliandaa fomu za kutolea mafuta ambapo kwa kushirikiana na Simon Lemeya Tukai na Simaloy Baby Lemeya mfanyakazi wa kituo cha mafuta cha Simon Lemeya pamoja na Ally Sadick wa kituo cha Membi Filling Station, walighushi saini za madereva,” inaeleza taarifa ya Makungu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!