Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya wa Chadema Iringa ang’olewa
Habari za Siasa

Meya wa Chadema Iringa ang’olewa

Alex Kimbe, aliyekuwa Meye wa Iringa
Spread the love

ALEX Kimbe, Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo tarehe 28 Machi 2020, ameondolewa madarakani na Baraza la Madiwani la halmashauri hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa … (endelea).

Hatua hiyo imechukuliwa katika kikao maalumu cha baraza la madiwani kilichoketi leo, kwa ajili ya kujadili tuhuma zilizokuwa zinamkabili Meya Kimbe, ikiwemo za matumizi mabaya ya madaraka na mamlaka.

Meya Kimbe ameondolewa madarakani kwa kura za ndio 14 kati ya 26, zilizopigwa na wajumbe katika kikao hicho.

Kwa mujibu wa Hamid Njovu, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa, Meya Kimbe ameondolewa madarakani, baada ya Tume ya Uchunguzi dhidi yake iliyoundwa na Ally Hapi, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, kumkuta na hatia.

Njovu amedai kuwa, Meya Kimbe aliamuru baadhi ya wajumbe wa halmashauri hiyo, kufanya ziara mkoani Mbeya na Njombe, pasipo kupata kibali cha Mkuu wa Mkoa.

“Amekuwa akitumia nafasi yake vibaya ya madaraka na mamlaka, matokeo ya uchunguzi ni kama ifuatavyo, kuamuru wajumbe wa halamshauri kufanya ziara pasipo kupata kibali cha mkuu wa mkoa,” amedai Njovu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!