Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya wa Chadema aliyejiuzuru Iringa, avuliwa uanachama
Habari za SiasaTangulizi

Meya wa Chadema aliyejiuzuru Iringa, avuliwa uanachama

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoa wa Iringa kimemvua uanachama Dady Igogo aliyekuwa diwani wa Kata ya Gangilonga na Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa baada ya kukutwa na kosa la kukisaliti chama. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii huku ikionesha imetolewa na Katibu wa Chadema Jimbo la Iringa Mjini, Suzana Mgonokulima, imeeleza kuwa Kamati Tendaji ya Jimbo imechukua uamuzi huo baada ya kumkuta mtuhumiwa kwa makosa ya kukisaliti chama, kujivua nafasi ya Unaibu Meya na baadaye Udiwani.

Taarifa kamili iliyotolewa na Chadema Jimbo la Iringa Mjini hii hapa:-

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) JIMBO LA IRINGA MJINI :

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NA UMMA.

YAH: KUFUKUZWA UANACHAMA NDUGU DADY JOHANES IGOGO:

Dady Igogo aliyekuwa Diwani wa CHADEMA kata ya Gangilonga na Naibu Meya Manispaa ya Iringa; alikisaliti Chama na kujivua nafasi ya Unaibu Meya na baadaye Udiwani kwa kile alichokiita “Sababu zilizoko moyoni mwake.”

Katiba ya CHADEMA 2006 , Toleo la 2016 Ibara 5.4. Inaeleza na kufafanua juu ya “kukoma kwa uanachama.”

Vile vile Ibara 5.4. (1 , 2, na 3) inaeleleza kuwa mwanachama atakoma uanachama wake kwa kujiuzulu , kufariki , kuachishwa ama kufukuzwa.

Ndugu Igogo kwa muda mrefu amekuwa na mwenendo usioendana na Itikadi, Falsafa, Madhumuni, Kanuni, Maadili na Sera za Chama.

Kamati tendaji ya Jimbo katika kikao chake cha dharura kilichoketi Tar.24/04/2018 kiliazimia yafuatayo:

1. Dady Igogo avuliwe ujumbe wa kamati tendaji ya Jimbo kwa mujibu wa Ibara 7.4.10 (x) na Ibara 7.7.8 (k) kwa kwenda kinyume na katiba ya chama, kanuni na maadili ya chama.

2. Dady Igogo afukuzwe uanachama kwa mujibu wa Ibara 5.4.3 kwa kuwa amekosa sifa za kuendelea kuwa mwanachama wa CHADEMA.

Hivyo kuanzia leo tar 28/04/2018 Chama kinatoa taarifa kwa wanachama na umma kuwa Dady Igogo sio mwanachama wa CHADEMA tena.

Imetolewa na;

Suzana Mgonokulima.

Katibu wa CHADEMA.

Jimbo la Iringa Mjini.

27/04/2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!