Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Meya Londa ajisalimisha Urafiki
Habari Mchanganyiko

Meya Londa ajisalimisha Urafiki

Meya wa zamani wa Manispaa ya Kinondoni Alhaji Salum Londa
Spread the love

ALIYEKUWA Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Alhaji Salum Salehe Londa, amelipa deni la pango ya nyumba, analodaiwa na kiwanda cha Nguo cha Urafiki, anaandika Hamisi Mguta.

Taarifa kutoka ndani ya shirika hilo zinasema, Londa alifika makao makuu ya kiwanda hicho yaliyopo maeneo ya Urafiki, barabara ya Morogoro, Ubungo jijini Dar es Salaam, majira ya saa tisa jioni ya leo Jumatano kulipa deni lake.

Londa anadaiwa na kampuni hiyo kiasi cha Sh. 18 milioni ikiwa ni pango la nyumba anayoishi iliyopo eneo la Makaburini, Kinondoni.

Mwandishi wa habari hii, alikutana na Londa ndani ya kiwanda hicho akielekea sehemu ya malipo ili kulipa deni lake.

Habari zinasema Meya Londa amelipa fedha zote Sh. 18 milioni alizokuwa anadaiwa na kiasi gani katika deni analodaiwa na kampuni ya Urafiki.

Awali taarifa zinasema, kampuni hiyo kupitia wakala wake wa kukusanya madeni – Yono Action Mart – ilitoa hadi saa tisa jioni ya leo kwa mwanasiasa huyo wa zamani kulipa deni, vinginevyo angefukuzwa kwenye nyumba hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!