Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Meya Iringa njia panda, mahakama yamtosa
Habari za Siasa

Meya Iringa njia panda, mahakama yamtosa

Alex Kimbe, Meya wa Manispaa ya Iringa
Spread the love

MAHAKAMA ya Mkoa wa Iringa, imetupilia mbali ombi la Alex Kimbe, Meya wa Manispaa ya Iringa la kuzuia mchakato wa kumng’oa madarakani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Iringa…(endelea).

Uamuzi huo umetolewa leo tarehe 27 Machi 2020 na mahakama hiyo mbele ya Aden Kanje, Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Kanje amesema, ombi hilo limetupwa kutokana na kuwa na makosa, kitendo kilichopelekea mahakama hiyo kushindwa kusikiliza kesi hiyo kwa mujibu wa sheria.

Awali kikao cha kuendesha mchakato wa kumng’oa Meya Kimbe jana tarehe 26 Machi 2020, kilikwama baada ya madiwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutohudhuria.

Hata hivyo, Hamid Njovu, Mkurugenzi wa Halmshauri ya Manispaa ya Iringa, ameitisha Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani la manispaa hiyo, kesho tarehe 28 Machi 2020.

Miongoni mwa ajenda ya kikao hicho kesho, ni kupiga kura ya kutokuwa na imani na Meya Kimbe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!