Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Membe, Musiba kukutana Julai 2
Habari Mchanganyiko

Membe, Musiba kukutana Julai 2

Spread the love

MAKAHAMA Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam imepanga tarehe 2 Julai 2019 kutoa uamuzi wa madai ya fidia ya Sh. 10 bilioni, ya kesi iliyofunguliwa na Bernard Membe, waziri wa zamani wa Mambo ya Nje dhidi ya Cyprian Musiba. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).  

Mahakama hiyo mbele ya Jaji Jocqwine Demela leo tarehe 17 Mei 2019, imepanga tarehe hiyo baada ya mawakili wa pande zote mbili,  Wakili Majura Magafu anamtetea Musiba na Wakili Johnathan Mndeme anayemwakilisha Membe, kusikilizwa hoja zao.

Upande wa walalamikiwa uliwasilisha maombi namna 119/2019 ya kuomba kuongezewa muda wa kuwasilisha majibu yake nje ya muda.

Katika kesi hiyo Musiba, anayejitambulisha kama mwanaharakati na mtetezi wa Serikali na Rais John Magufuli, anatuhumiwa na Membe kwamba, anamhujumu Rais Magufuli, ikiwa ni pamoja na kufanya kampeni za kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!