BERNARD Kamilius Membe, mgombea urais wa Tanzania kupitia chama cha ACT-Wazalendo, anarejea nchini mwake kesho Jumanne tarehe 15 Septemba 2020 akitokea Dubai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)
Membe aliondoka nchini Tanzania hivi karibuni kwenda Dubai ikiwa ni siku chache kupita tangu alipozindua kampeni zake za urais mkoani Lindi na kufanya mikutano kadhaa mikoa ya Mtwara na Pwani.
Mwanadiplosia huyo mashuhuri aliyepata kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kuanzia mwaka 2007 hadi 2015, ametumia ukaunti yake ya Twitter kuelezea safari yake.
Wana ACT- Wazalendo na Watanzania wenzangu wote! Kesho Jumanne ya tarehe 15 Sept.saa 8.40 mchana, nitatua DSM nikitokea Dubai na nitafanya Press Conference Airport. Afya yangu imeimarika na sasa nipo tayari kwa Kampeni ya Urais inayoanzia Tabora wiki hii hadi October 26.
— Bernard K. Membe (@BenMembe) September 14, 2020
“Wana ACT- Wazalendo na Watanzania wenzangu wote! kesho Jumanne ya tarehe 15 Sept.saa 8.40 mchana, nitatua DSM nikitokea Dubai na nitafanya Press Conference Airport.”
“Afya yangu imeimarika na sasa nipo tayari kwa kampeni ya Urais inayoanzia Tabora wiki hii hadi 26 Oktoba 26,” ameandika Membe ambaye pia ni Mshauri Mkuu wa ACT-Wazalendo.
Leave a comment