Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Membe atajwa Mkutano mkuu ACT-Wazalendo
Habari za SiasaTangulizi

Membe atajwa Mkutano mkuu ACT-Wazalendo

Spread the love

JINA la Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje Mstaafu, limetajwa katika Mkutano Mkutano Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, unaoendelea katika Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Jina hilo limetajwa leo tarehe 14 Machi 2020 na Dk. Azaveli Lwaitama, wakati akizungumzia hoja ya upatikanaji wa mgombea binafsi wa urais.

Dk. Lwaitama amelitaja jina la Membe kipindi ambacho mwanasiasa huyo amefurushwa katika Chama chake cha Mapinduzi (CCM), kwa kosa la utovu wa nidhamu.

Hata hivyo, Membe anadai hatua ya kufukuzwa CCM inatokana na harakati zake, za kutaka kugombea urais kwenye uchaguzi ujao kupitia chama hiko.

Kufuatia sakata hilo, Dk. Lwaitama amewaeleza wajumbe wa mkutano huo kuwa, kama sheria za nchi zingeruhusu mgombea binafsi, Membe asingehangaika kutafuta fursa ya kugombea Urais wa Tanzania kupitia vyama vya siasa.

Mwanazuoni huyo ameeleza kuwa, kutokuwepo kwa fursa hiyo, kunaweza pelekea Membe kuhangaika katika vyama vingine vya siasa pasina mafanikio, kisha kurejea katika Chama chake cha CCM.

“Bila ya kuwa na nguvu ya umma huwezi kuwa na mgombea huru, kusudi Membe awe na akili nzuri zaidi ya kugombea badala ya kuhangaika huko, baadae kurudi nyumbani,” amesema Dk. Lwaitama.

Wakati huo huo, Dk. Lwaitama ameshauri sheria ya uchaguzi kurekebishwa, ili kuruhusu mgombea binafsi wa urais, kwa kuwa hilo lilikua takwa la Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Amesema Mwalimu Nyerere alikufa akipigania nchi kuwa na sheria inayoruhusu mgombea binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!