Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto amteua Membe kuwa mshauri mkuu ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Zitto amteua Membe kuwa mshauri mkuu ACT-Wazalendo

Bernard Membe
Spread the love

BERNARD Membe, mwanachama mpya wa Chama cha ACT-Wazalendo, amepewa cheo cha ‘mshauri wa chama’ hicho. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Kabla ya Membe, cheo hicho kilikuwa cha Maalim Seif Sharif Hamad, ambapo baada ya kugombea na kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa chama hicho Taifa, nafasi ya mshauri wa chama ilibaki wazi.

Zitto Kabwe, kiongozi wa chama hicho ndiye aliyependekeza cheo hicho kwa Membe kwenye kikao cha wajumbe wa Halmashuri Kuu kinachofanyika leo tarehe 3 Agosti 2020, katika Ukumbi wa Mikutano wa Lamada jijini Dar es Salaam.

“Kuna nafasi zilizo wazi, miongoni mwazo ni nafasi ya mshauri wa chama, hivyo tunapendekeza Bernard Membe kuwa mshauri mkuu wa chama chetu,” Zitto aliwaeleza wajumbe wa kikao hicho.

Maalim Seif Sharif Hamad, Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo

Wajumbe hao walipokea kwa shangwe pendekezo hilo, huku wakipiga makofi kupongeza hatua ya Membe kupendekezwa kuwa mshauri wa chama hicho.

“Mheshimiwa mwenyekiti (Maalim Seif), kwa makofi na shangwe hizi, naona wajumbe wa Halmashauri Kuu wameridhia Membe kuwa mshauri wa chama chetu,” alisema Zitto.

Baada ya Membe kukubaliwa na Halmashauri Kuu kuwa mshauri wa chama hicho, Zitto alimwita jukwaani na kisha alipewa kiti.

Zitto alitoa pendekezo la Membe baada ya kuruhusiwa na mwendesha mkutano huo ambaye ni Maalim Seif. Membe alijiunga na chama hicho mwezi uliopita baada ya kufutiwa uanachama wake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumzia hatua hiyo, Janeth Rite ambaye ni Naibu Katibu wa Uenezi na Mawasiliano ya Umma wa chama hicho amesema, Membe ameteuliwa kutokana na uzoefu wake katika medani za siasa za Tanzania.

“Membe ni mbobezi katika medani za siasa Tanzania, hiyo ni miongoni mwa sababu iliyokisukuma chama na wajumbe wa Halmashauri Kuu kuridhia uteuzi huo,” amesema Janeth.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!