Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Membe achukua fomu kuwania urais Tanzania
Habari za Siasa

Membe achukua fomu kuwania urais Tanzania

Spread the love

BERNARD Kamilius Membe, Mgombea Urais wa Tanzania kupitia chama cha ACT-Wazalendo, amechukua fomu ya kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Membe ambaye ni Mshauri Mkuu wa chama hicho, amekabidhiwa fomu hizo leo Ijumaa tarehe 7 Agosti 2020, Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji mstaafu Semistocles Kaijage

Membe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania katika utawala uliopita chini ya Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete aliongozana na mgombea mwenza, Profesa Omar Fakih Hamad.

          Soma zaidi:-

Pia, wamesindikizwa na viongozi wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad (mwenyekiti) na Katibu Mkuu wake, Ado Shaibu.

Juzi Jumatano, mkutano mkuu wa ACT-Wazalendo ulimteua Membe kugombea urais kwa kupata kura 410 sawa na asilimia 97 ya kura zote 420. Kura za wajumbe 10 zilimkataa.

Shughuli ya uchukuaji na urejeshaji wa fomu hizo ulianza tarehe 5 utahitimishwa 25 Agosti 2020.

Kampeni za uchaguzi mkuu zitaanza 26 Agosti hadi 27 Oktoba 2020 na Uchaguzi Mkuu utafanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!