KIVUKO cha MV. Nyerere kinachotoa huduma kati ya Ukara na Bugorola wilayani Ukerewe mkoa wa Mwanza kimezama mchana wa leo tarehe 20 Septemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa hiyo imetolewa kwa vyombo vya habari na Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA).
Akizungumzia kuhusu tukuio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, ACP Jonathan Shana amesema baadhi ya wau waliokuwamo katika kivuko hicho kilichokuwa kinatoka Bugorora kisiwani Ukerewe kuelekea Kisiwa cha Ukara, wameanza kuokolewa.
Kamanda Shana amesema shughuli za uokoaji wahanga zinaendelea kutekelezwa na Kamati ya Ulinzi na usalama mkoa wa Mwanza.
Leave a comment