Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mei Mosi: Zitto apasuka
Habari za SiasaTangulizi

Mei Mosi: Zitto apasuka

Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo amepinga sababu zilizotolewa na Rais John Magufuli za kutopandisha mishahara ya Watumishi wa Umma kwa miaka minne mfululizo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza leo tarehe 1 Mei 2019, jijini Dar es Saalam, Zitto amesema Serikali zote zilizopita zilifanya miradi ya maendeleo sambamba na kupandisha mishahara ya Wafanyakazi.

Zitto ametoa msimamo huo saa chache baada ya Rais Magufuli kueleza kwamba Serikali yake haipandishi mishahara ya watumishi wa umma kwa sababu inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, kwa minajili ya kumpunguzia mfanyakazi gharama za maisha.

Akihutubia wananchi katika maazimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani ‘Mei Mosi’ jijini Mbeya, Rais Magufuli amesema Serikali inakabiliwa na changamoto ya gharama za uendeshaji ikiwemo kulipa watumishi mishahara, deni la taifa, pamoja na kutekeleza miradi ya maendeleo. Na kuahidi kwamba miradi ya maendeleo ikikamilika itachochea ukuaji wa uchumi na kupunguza ukali wa gharama za maisha.

Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini, amepinga sababu hizo huku akirejea Serikali za awamu zilizopita kwamba licha ya kutekeleza miradi ya maendeleo lakini zilikuwa zinapandisha madaraja, mishahara pamoja na kulipa stahiki za watumishi wa umma.

“Kwa nini Serikali isiwaambie ukweli wananchi kwamba imeshindwa kuongeza mshahara kwa sababu hali ya uchumi ni mbaya, gharama za uendeshaji serikali zimeongezeka na gharama ya kulipa deni la taifa imeongezeka badala ya kusingizia miradi?” Amehoji Zitto na kuongeza.

“Serikali hii ilikua ikiisema serikali ya awamu ya nne kulikuwa na ufisadi, ubadhirifu wa fedha za umma, vyeti feki pamoja na watumishi hewa na ukwepaji kodi, lakini serikali hiyo iliweza kupandisha mishahara kwa mujibu wa sheria. Alivyoingia madarakani Rais Magufuli aliondoa watumishi hao na kuzuia ufisadi, iweje ashindwe kuongeza mishahara?”

Zitto amesema nchi inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo bila kutumia maarifa na kujiandaa vyema, hali inayoathiri ukuaji wa pato la taifa na kupelekea Serikali kushindwa pandisha mishahara ya watumishi wake.

“Hapa kwetu tunatekeleza miradi mikubwa lakini pato la taifa linaporomoka kwa sababu tumetekeleza bila kutumia maarifa ya kutosha, malighafi za ndani zinazowezakana na kuandaa wananchi. Matokeo yake miradi badala ya kuchochea ukuaji wa uchumi, inasababisha uchumi kutokuwa kwa kasi,” amesema Zitto.

Aidha, Zitto ameishauri Serikali kuhakikisha kwamba shughuli za kiuchumi zinaimarika ikiwemo kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji na ufanyaji biashara, ili kutengeneza fursa nyingi za ajira za kudumu na kuiwezesha serikali kupata mapato kupitia kodi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!