MDOGO wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche aitwaye Chacha Heche Suguta, adaiwa kuuwawa akiwa chini ya Jeshi la Polisi baada ya kukutwa akiwa jeraha la kuchomwa kisu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Ndugu wa marehemu wanasema wakati alipokamatwa na Polisi alikuwa mzima kabisa. Muda huu mabomu ya machozi na risasi vinafurumushwa kuwafukuza wananchi kutoka kituoni.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, RPC Mwibambe amekiri askari wake kuhusika na mauaji hayo ya kijana huyo aliyezaliwa mwaka 1989. Chacha Suguta ni mdogo (upande wa Baba mdogo) wa Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (Chadema).
John Heche anasema kuwa kijana huyo alikamatwa na Askari wa Jeshi la Polisi usiku wa jana akiwa Baa akiwa mzima kabisa.
Watu hawako salama tena mikononi mwa polisi. Mdogo wangu Suguta amekamatwa na polisi jana usiku na ameuwawa na polisi kwa kuchomwa kisu. Najisikia maumivu mno, hii sio nchi ambayo tunaitaka. Najiuliza maswali mengi ni kwa vipi mtu amefungwa pingu anachomwa kisu tena na polisi.
— John Heche (@HecheJohn) April 27, 2018
Heche amesisitiza kuwa baada ya kufariki, Askari wa Polisi walitaka kuutupa mwili wake lakini ilishindikana kwa sababu eneo walilotegemea kuutupa kulikuwa na Mlinzi aliyewafukuza, ndipo walipoamua kuupeleka mwili wake kwenye chumba cha kuhifadhia maiti (Mortuary) ya Tarime.
Leave a comment