Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee, Bulaya, Matiko kuwa huru leo
Habari za Siasa

Mdee, Bulaya, Matiko kuwa huru leo

Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimelipa hukumu ya faini ya Sh. 100 milioni katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa ajili ya kuwakomboa viongozi wake wa kike. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea)

Hayo amesema Said Mohammed, Kaimu Mwenyekiti wa Chadema, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Mohammed amesema watakaolipiwa faini ni Halima Mdee, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha), Esther Matiko, Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Serengeti na Esther Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini.

Amesema, Mdee amelipiwa faini ya Sh. 40 milioni, wakati Matiko akilipiwa faini ya Sh. 30 milioni,  huku Bulaya akilipiwa faini ya Sh. 30 milioni.

Mohammed amesema kwa sasa mawakili wa chama hicho wanafuatilia kibali cha mahakama cha kuwatoa gerezani viongozi hao.

“Milioni 100 imetumika kwa maana tumepata kodi namba ya washtakiwa wetu, tumeenda kulipia. Tunasubiri mawakili kupata remove oda kwa ajili ya kumtoa Mdee gharama yake ni milioni 40 imelipwa. Matiko Milioni 30 imelipwa na Bulaya milioni 30 tumeshalipa,” amesema Mohammed na kuongeza:

“Tunategemea sana mawakili wetu wataweza kufanikisha leo hii na tutaungana nao ili kusaidiana nao kusuma ili lutoa viongozi waliobakia.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!