Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee aweka msimamo Kawe 2020
Habari za Siasa

Mdee aweka msimamo Kawe 2020

Halima Mdee, aliyekuwa ubunge wa Kawe kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

HALIMA Mdee, Mbunge wa Kawe, jijini Dar es Salaam amesema, hakuna wa kumbabaisha kwenye Jimbo la Kawe, kuelekea uchaguzi mkuu wa 2020. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Mdee ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA) amesisitiza, mtu wa kumng’oa katika Jimbo la Kawe, hajazaliwa.

Ametoa kauli hiyo leo tarehe 8 Januari 2020, alipoulizwa na MwanaHALISI Online kwamba, inaeleza kuwa na hofu ya kushindwa kwenye jimbo hilo.

Na kwamba, taarifa zinaeleza kuwa hana mpango wa kugombea kwenye jimbo katika uchaguzi mkuu wa 2020, hivyo karata pekee ya kumfanya kuwa mbunge ni kupitia Viti Maalum akiwa Mwenyekiti BAWACHA.

“…mpaka sasa hakuna wa kuniondoa Kawe, hajazaliwa mpaka sasa,” Mdee amesema kwa kifupi akidai, wakati wa kutoa maelezo marefu kuhusu swali hilo, haujafika.

Mdee pia amekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutorudia iliyofanya kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, kwamba hakitavumilika tena.

“Wasije wakafikiria uhuni wa serikali za mitaa wataufanya kwenye uchaguzi wa madiwani na wabunge. Kwanza huko chini hakukaliki. Wamejipa vyeo kinadharia lakini vitendo Chadema ndio mpango mzima kitaa,” amesema Mdee.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!