Friday , 29 March 2024
Habari za Siasa

Mdee atoka mahabusu

Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Kagera, limemwacha kwa dhamana Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), Halima Mdee. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Jeshi hilo lilimshikilia Mdee ambaye pia ni Mbunge wa Kawe, tangu jana tarehe 14 Julai 2019, kwa tuhuma za kufanya uchochezi.

Mdee, Grace Tendega, Katibu wa Bawacha; Conchesta Rwamlaza, Mwenyekiti wa Bawacha Mkoa wa Kagera na Anatropia Theonest; Mbunge Viti Maalum jana walikamatwa na kuhojiwa ambapo Mdee pekee hakupewa dhamana.

Awali, Polisi waligoma kumpa dhamana Mdee wakidai wanasubiri maelekezo kutoka kwa Kamanda wa Mkoa wa Kagera, aliyekuwa kwenye ziara ya Rais John Magufuli.

Taarifa iliyotolewa Chadema imeeleza kuwa, Mdee amedhaminiwa na watu wawili ambapo pia ametakiwa kuripoti kituoni hapo baada ya mwezi mmoja au wakati wowote polisi watakapomuhitaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!