Tuesday , 23 April 2024
Habari za Siasa

Mdee ampuuza Ndugai

Job Ndugai,. Spika wa Bunge la Tanzania
Spread the love

HALIMA James Mdee, Mbunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amesema kauli ya Job Ndugai kwamba wabunge waliopewa adhabu hawatarudi bungeni hata wakienda mahakamani ni ya kupuuzwa, anaandika Irene Emmanuel.

Mdee ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (Bawacha) amesema Ndugai amekuwa akiliendesha Bunge kwa upendeleo wa wazi, huku wabunge  wa chama tawala wakiwa hawachukuliwa hatua wanapokosea.

Akizungumza, katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya Chadema, jijini Dar es salaam Mdee amesema, “Ndugai anatapatapa na hivyo mimi nitaendelea  kumpuuza, kama ambavyo nimekua nikimpuuza.

“Mahakama inafanya kazi yake, na endapo malalamiko yangu yakionekana hayana mantiki basi nitaendelea kutumikia adhabu niliyopewa.”

Itakumbukwa kuwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilitoa uamuzi wa kuwafungia Mdee na Esther Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini kuhudhuria vikao vya bunge kwa kipindi cha mwaka mmoja kutokana na kile kilichotajwa kuwa ni utovu wa nidhamu ndani ya bunge.

Hata hivyo, Mdee ameiambia MwanaHALISI online, “sisi tumeenda kudai haki yetu kupitia Mahakama Kuu, ambayo imepewa mamlaka yasiyo na kikomo kushughulikia masuala ya kisheria.

“Mahakama itafanya kazi yake na itatoa haki. Bunge halipo juu ya Katiba, Mahakama jukumu lake ni kutoa haki, Spika asidhani yeye yupo juu ya Katiba.”

Wiki iliyopita Spika Ndugai alilieleza Bunge kuwa wabunge waliosimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge (Mdee na Bulaya) hawatarudi bungeni kabla ya mwaka mmoja wa adhabu kuisha hata kama wataenda katika mamlaka zingine kudai haki.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!