Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa MCT wamtia hatiani Makonda
Habari za SiasaTangulizi

MCT wamtia hatiani Makonda

Katibu Mkuu wa MCT, Kajubi Mukajanga. Picha ndogo, Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam
Spread the love

BARAZA la Habari Tanzania (MCT), limezidi kumkaanga Mkuu wa Dar es Salaam, Paul Mkaonda baada ya kubaini kwamba alihusika moja kwa moja kuvamia Clouds Media Group, anaandika Faki Sosi.

Mwezi Machi mwaka huu, Tume maalum iliyoundwa na aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ilitoa ripoti kama ya MCT.

Katika ripoti yake, MCT imebaini Makonda alihusika kufanya uvamizi huo na wamejiridhisha pasipo kuacha shaka na kwamba hawajamuonea.

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga amesema kuwa ripoti hiyo hajamuonea Makonda.

“Hatujafanya utafiti huu kwa sababu tunamahaba maalum na Clouds au tunamahaba na mkuu wa mkoa na kwamba huu sio utafiti wa kwanza tulianza kwa marehemu Daudi Mwangosi alipouwa,” amesema

”Sisi kwetu haijarishi watu wameelewana au hawajaelewana sisi kwetu tunaangalia uvamizi huu jinsi ilivyoathiri vyombo vya habari”, amesema Mukajanga

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!