Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa  Mchungaji Msigwa awavaa wanaoikosoa Chadema
Habari za Siasa

 Mchungaji Msigwa awavaa wanaoikosoa Chadema

Mch. Peter Msigwa
Spread the love

MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini amewashukia wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wanao kikosoa chama hicho mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 16 Desemba 2019, Mchungaji Msigwa amewashauri wafuasi wa Chadema wenye maoni juu ya chama hicho, kupeleka ushauri wao kwenye vikao vya chama.

Mwenyekiti huyo wa Chadema Kanda ya Nyasa, amewashangaa wanachama hao wanaoshindwa kufikisha ushauri wao katika vikao vya chama, na badala yake wanapeleka madukuduku yao mitandaoni.

“Kuna vikao ambavyo vinaanzia kwenye msingi kwa sisi Chadema, mpaka taifa. Sasa wewe kama ni Mwana Chedema, kama una ushauri anzia huko.

Lakini wengi hawataki kuhudhuria huko , ila kwenye mitandao ndio mafundi wa kukosoa. Chama lazima kiwe na nidhamu, Chama ni vikao, lazima tuheshimu,” ameandika Mchungaji Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!