TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Manyara, inamshikilia Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Kiinjili la Kulutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Ufana, Emanuel Petro Guse kwa kuendesha mikopo umiza bila ya leseni ya biashara ya ukopeshaji fedha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)
Taarifa ya Mkuu wa Takukuru, Mkoa wa Manyara, Holle Makungu aliyoitoa leo Ijumaa tarehe 28 Agosti 2020 imesema, wanaendelea kumshikilia kwa uchunguzi zaidi wa mikataba umiza 48 iliyokutwa nyumbani kwake wakati wa upekuzi.
Taarifa yote ya suala hilo hii hapa;
Leave a comment