Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mchungaji Kenya ahukumiwa miaka 75 jela
Habari Mchanganyiko

Mchungaji Kenya ahukumiwa miaka 75 jela

Spread the love

ASKOFU katika kaunti ya Kisumu nchini Kenya, Joseph Agutu amehukumiwa kifungo cha miaka 75 jela baada ya mahakama kumkukuta na hatia ya kuwabaka watoto wa kike watatu, huku mmoja kati yao akimuambikiza Virusi vya Ukimwi(VVU). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hukumu hiyo ilitolewa jana tarehe 18 Desemba 2018 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Pauline Mbulika baada ya ushahidi uliotolewa na mmoja kati ya mashahidi katika kesi hiyo, kuthibitisha kwamba askofu huyo alifanya ngono zembe zaidi ya mara tano kwa watoto hao.

Agutu alihukumiwa kifungo hicho na mahakama kutokana na makosa manne yaliyokuwa yakimkabili, ambapo alitenda katika nyakati tofauti kwenye kipindi cha mwezi Aprili na Julai mwaka 2016 katika eneo la Kachok.

Katika makosa hayo, Askofu huyo alishtakiwa kwa kumuambukiza VVU kwa makusudi mtoto mmoja. Agutu amefungwa miaka 20 jela kwa kila kosa katika makosa matatu, wakati kosa la nne akifungwa miaka 15.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!