ASKOFU katika kaunti ya Kisumu nchini Kenya, Joseph Agutu amehukumiwa kifungo cha miaka 75 jela baada ya mahakama kumkukuta na hatia ya kuwabaka watoto wa kike watatu, huku mmoja kati yao akimuambikiza Virusi vya Ukimwi(VVU). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Hukumu hiyo ilitolewa jana tarehe 18 Desemba 2018 na Hakimu Mkazi Mwandamizi, Pauline Mbulika baada ya ushahidi uliotolewa na mmoja kati ya mashahidi katika kesi hiyo, kuthibitisha kwamba askofu huyo alifanya ngono zembe zaidi ya mara tano kwa watoto hao.
Agutu alihukumiwa kifungo hicho na mahakama kutokana na makosa manne yaliyokuwa yakimkabili, ambapo alitenda katika nyakati tofauti kwenye kipindi cha mwezi Aprili na Julai mwaka 2016 katika eneo la Kachok.
Katika makosa hayo, Askofu huyo alishtakiwa kwa kumuambukiza VVU kwa makusudi mtoto mmoja. Agutu amefungwa miaka 20 jela kwa kila kosa katika makosa matatu, wakati kosa la nne akifungwa miaka 15.
Leave a comment