Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mch. Msigwa aweka rehani ubunge wake kisa Makonda
Habari za SiasaTangulizi

Mch. Msigwa aweka rehani ubunge wake kisa Makonda

Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini
Spread the love

MBUNGE wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema yupo tayari kujiuzuru ubunge wake kama itathibitika kuwa amemtelekeza mtoto kwa mwanamke mmoja jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwanadishi Wetu … (endelea).

Mch. Msigwa ametajwa na mwanamke mmoja kati ya walioripoti katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuwa ametelekeza mtoto.

Makonda ametoa nafasi kwa wanawake waliotelekezwa na wanaume waliowazalisha, ndipo mwanamke huyo ambaye hajatajwa jina lake alifika katika ofisi za Mkuu wa Mkoa na kueleza kuwa amezalishwa na mbunge huyo na kumtelekeza bila matunzo yoyote.

Katika taarifa yake, Mch. Msigwa amesema kinachoelezwa kuwa ametelekeza mtoto jijini na mwanamke huyo ni propaganda za makusudi zenye lengo la kujaribu kumchafua.

Msigwa amesema: “Kama huyo mama ambaye jina lake limehifadhiwa yupo, nataka ajitokeze pamoja na mtoto niliyemtelekeza. Kwa sasa nipo Dodoma Bungeni; anaweza kunipata kupitia Spika wa Bunge au Katibu wa Bunge au Kiongozi wa Upinzani Bungeni.”

Mbunge huyo amesema kama ikithibitika kuna mtoto amemtelekeza yupo tayari kujiuzuru Ubunge.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!