MBUNGE wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema yupo tayari kujiuzuru ubunge wake kama itathibitika kuwa amemtelekeza mtoto kwa mwanamke mmoja jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwanadishi Wetu … (endelea).
Mch. Msigwa ametajwa na mwanamke mmoja kati ya walioripoti katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuwa ametelekeza mtoto.
Makonda ametoa nafasi kwa wanawake waliotelekezwa na wanaume waliowazalisha, ndipo mwanamke huyo ambaye hajatajwa jina lake alifika katika ofisi za Mkuu wa Mkoa na kueleza kuwa amezalishwa na mbunge huyo na kumtelekeza bila matunzo yoyote.
Katika taarifa yake, Mch. Msigwa amesema kinachoelezwa kuwa ametelekeza mtoto jijini na mwanamke huyo ni propaganda za makusudi zenye lengo la kujaribu kumchafua.
Msigwa amesema: “Kama huyo mama ambaye jina lake limehifadhiwa yupo, nataka ajitokeze pamoja na mtoto niliyemtelekeza. Kwa sasa nipo Dodoma Bungeni; anaweza kunipata kupitia Spika wa Bunge au Katibu wa Bunge au Kiongozi wa Upinzani Bungeni.”
Mbunge huyo amesema kama ikithibitika kuna mtoto amemtelekeza yupo tayari kujiuzuru Ubunge.
Leave a comment