Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge: Wageni hawaingii Tanzania kuhofia usalama wao
Habari za Siasa

Mbunge: Wageni hawaingii Tanzania kuhofia usalama wao

Frank Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma
Spread the love

MBUNGE wa Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema) amesema, Serikali imeshindwa kutatua tatizo la upatikanaji wa umeme katika mpaka wa Tunduma mkoani Songwe kwa muda mrefu jambo linalosababisha kupoteza wageni na wateja wa bandari ya Dar es Salaam kwa kuhofia usalama wao kutokana na giza. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kutokana na hali hiyo, Mwakajoka ameihoji  Serikali na kutaka kujua kama iko tayari kuunganisha umeme wa Zambia ili huduma ya nishati ya umeme iwe inapatikana muda wote ikiwa ni kulinda wateja wanaopitisha mizigo toka bandari ya Dar es Salaam na mpaka wa Tunduma.

Wizara ya Nishati ikijibu swali hilo ilisema, Mji wa Tunduma unatumia umeme wa Gridi ya Taifa kwa asilimia 100 kupitia njia ya msongo wa kilovoti 33 kutoka Kituo cha kupoza Umeme cha Iyunga, Mjini Mbeya na kusambaza umeme katika maeneo ya Wilaya za Mbozi, Momba na Songwe.

Imesema kwa ujumla, hali ya upatikanaji umeme kwa sasa ni ya kuridhisha, hata hivyo, hitilafu katika baadhi ya miundombinu ya umeme imekuwa ikisababisha kuzima umeme ili kupisha matengenezo katika njia kuu ya umeme katika Mkoa wa Songwe na baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Mbeya vijijini.

Katika majibu hayo, wizara hiyo imesema, Serikali kupitia TANESCO imekarabati miundombinu ya umeme ili kuimarisha upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo.

“Aidha, katika mwaka wa fedha 2020/21 TANESCO imepanga kujenga kituo cha umeme Mlowo (switching station) pamoja na njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 65 kutoka kituo cha kupoza umeme cha Iyunga Mbeya hadi Mlowo kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.2.

“Mradi huu unatarajia kuanza kutekelezwa Mwezi Julai, 2020 na kukamilika Mwezi Mei, 2021 kupitia Kampuni ya TANESCO M/S Electrical Transmission and Maintenance Company (ETDCO) Limited,” imesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!