Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge mwingine Chadema ang’oka
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge mwingine Chadema ang’oka

Spread the love

JINAMIZI la kukimbiwa na wabunge na madiwani linazidi kuitafuna Chadema, ambapo jana tarehe 30, 2018 Mbunge wa Monduli, Julius Kalanga kupitia chama hicho ametangaza kujivua uanachama na kuhamia chama tawala CCM, Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Uamuzi huo wa Kalanga unakuja ikiwa zimepita siku mbili tangu aliyekuwa Mbunge wa Ukonga, Mwita Waitara kutangaza kujivua ubunge, uanachama na nyadhifa zote alizokuwa nazo Chadema na kurudi CCM kwa kile alichodai kuwa Chadema hakuna demokrasia.

Taarifa iliyotolewa leo kwa umma na Idara ya Itikadi na Uenezi CCM, inaeleza kuwa, Kalanga amepokelewa rasmi na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Humphrey Polepole usiku wa kuamkia leo.

Hivi karibuni Polepole alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa kuna wabunge wawili kutoka Chadema watahamia CCM huku akisisitiza kwamba idadi ya wanaokiomba chama hicho tawala kujiunga nacho haihesabiki.

Polepole alidai kuwa, kukosekana kwa ushirikiano kutoka uongozi wa juu wa chama ni kati ya sababu zinazowakimbiza wanaohama Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!