Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Msigwa amshitaki RC Hapi kwa waziri
Habari za Siasa

Mbunge Msigwa amshitaki RC Hapi kwa waziri

Ally Hapi
Spread the love

MBUNGE wa Iringa Mjini, Peter Msigwa (Chadema) amemshitaki Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Hapi kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mch. Msigwa amesema kuwa, Hapi amekuwa akisababisha wataalamu wa afya kukimbia hivyo kukosesha wananchi wa Iringa huduma bora za afya.

Amefikisha mashitaka hayo bungeni alipokuwa akichangia hotuba ya wizara hiyo juu ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/20.

Amesema kuwa, ziara inayofanywa na Hapi imekuwa ni ya kuwadhalilisha wataalamu, jambo ambalo limesababisha wataalamu wengi wa afya kukimbia.

Mbali na watumishi wa idara ya afya kukimbia na kusababisha adha kubwa kwa wale wanaohitaji huduma, Msigwa ameitaka serikali ieleze kama watumishi wa umma ni sahihi kuingiliwa na watendaji wa kisiasa.

Msigwa amesema kuwa, inasikitisha kuona viongozi wa kisiasa kugeuka kuwa mwiba kwa watumishi wa umma, kwa kutumia majukwaa kuwadhalilisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!