MBUNGE wa Jimbo la Ubungo (Chadema), Saed Kubenea amemtaka mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), anayetambulika na Msajili wa Vyama Vya Siasa Nchini Profesa Ibrahim Lipumba kuacha kulipotezea muda Jeshi la Polisi na kwamba aliache lifanye kazi yake , anaandika, Irene David.
Kauli hiyo ya Kubenea ikiwa ni siku moja baada ya Profea Lipumba kukimbilia Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam, akilalamika kwamba anatishiwa na mwanasiasa kutolewa katika ofisi yake iliyopo Buguruni jijini Dar es Salaam.
Wasiwasi huo umeibuka mara baada ya Uongozi wa Kanda ya Pwani na Dar es salaam (Chadema) na viongozi wa CUF wanaomuuunga mkono Maalim Seif wakiongozwa na Kubenea, wiki iliyopita kuanzisha operesheni ya Ondoa Msaliti Buguruni(OMB), kwa lengo la kumng’oa Profesa Lipumba ambaye ni msaliti.
Akizungumza na MwanaHALISI Online, Kubenea amesema amepokea wito wa polisi kwa njia ya simu na kwamba kesho mchana ataripoti polisi, lakini pia ameongeza kuwa kwa namna yoyote ile hatayumbishwa mpaka ahakikishe wanamng’oa ofisini msaliti huyo.
“Bado adhima ya kumwondoa msaliti Buguruni ipo palepale na haiwezi kurejeshwa nyuma kwa maneno rejareja na ahadi za uongo ama vitisho vya aina yoyote,”
“Lipumba ni msaliti ni lazima aondoke na katika hili ntauza hata kiatu changu lakini ataondoka.” amesema Kubenea.
Pomoja na hayo kubenea amesema, tayari matawi ya Chechinia, Hosigofina, Palestine, Kosovo, Saratoga, Arafati yote yameonyesha nia ya kumuunga mkono
Leave a comment