Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Kisangi: Uhaba shule za walemavu ni kikwazo
Habari za Siasa

Mbunge Kisangi: Uhaba shule za walemavu ni kikwazo

Spread the love

MBUNGE Viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam, Mariam Kisangi ameishauri serikali kuongeza idadi ya shule za watoto wenye mahitaji maalumu, akisema wengi wao wanakosa elimu kutokana na changamoto ya uhaba wa shule hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza bungeni Jijini Dodoma leo tarehe 31 Mei 2019 Mariamu amesema kume kuwepo na ongezeko la watoto wenye mahitaji maalum, na kwamba shule zilizopo hazina uwezo wa kubeba idadi hiyo.

“Kumekuwa na ongezeko la watoto wenye mahitaji maalum, kwa kuwa shule maalum zilizopo zinakuwa hazitoshelezi mahitaji, serikali haioni sababu ya kuongeza vitengo vya watoto wenye mahitaji maalum ili na wao waweze kupata elimu kwenye maeneo wanayotoka?” amehoji Mariam.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mwita Waitara amesema serikali imekwisha toa agizo kwa halmashauri nchini kuhakikisha kwamba wanajenga  miundombinu rafiki kwa watoto wenye uhitaji kwenye shule zilizopo nchini.

“Baada ya kuona unapotenga shule maalum unakuwa unawatenga, sasa imekuja elimu jumuishi, na tumetoa agizo kwenye ujenzi wa miundombinu iweke miundombinu ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu, na wanafunzi wawaone kuwa hao ni wenzao, na tunaongeza nguvu na ombi lako tutalifanyia kazi,” amejibu Waitara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!