Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Kabati: Mchungaji Msigwa ana bahati
Habari za Siasa

Mbunge Kabati: Mchungaji Msigwa ana bahati

Spread the love

RITA Kabati, Mbunge wa Viti Maalum (CCM) mkoani Iringa amesema, mambo mengi anayozungumza Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini, yanatekelezwa na serikali. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online kuhusu maendeleo ya jimbo hilo analotoka Kabati amesema, Serikali ya CCM imekuwa ikifanyia kazi hivyo jimbo hilo kupiga hatua.

“Mimi naingia Jimbo la Iringa Mjini ambalo mbunge wangu wa jimbo ni Mchungaji Msigwa, ana bahati kwasababu vitu vingi sana nimekuwa nikivisema na vimefanyiwa kazi na Serikali ya Chama cha Mapinduzi,” amesema.

Kabati amesema, walipoingia bungeni kulikuwa na tatizo la msongamano wa wagonjwa kwenye Hospitali ya Mkoa wa Iringa, ambapo alisimamia hoja ya upatikanaji wa Hospitali ya Wilaya ambapo iimepatikana.

“Naweza kusema, nimechangia sana kuwepo Hospitali ya Wilaya kwasababu, niliisemea na kuhakikisha inasajiliwa na inaanza kufanya kazi na mpaka leo, bado naisemea iweze kulaza hata wagonjwa,” amesema.

Hata hivyo Kabati  amesema, amepambana kuhakikisha wanahuisha Msitu wa Kihesa ambao ulikuwa chini ya halmashauri ili kutumia viwanja vya msitu huo kwa utalii.

“Kitovu cha Utalii Nyanda za juu Kusini kipo Iringa na tushukuru kwamba, hata uwanja wa ndege safari hii Bombardier itatua kwasababu tuliipigania sana,” amesema.

Amesema kuwa, kutoka na juhudi zake anazozifanya, amelisemea suala la machinjio ambayo imekuwa haipatiwi pesa kwa ajili ya kuyaendeleza hivyo mwaka huu, wamepatiwa Sh. 1.1 Bilioni  kwa ajili ya kuyaendeleza na kuwa chanzo kikubwa cha mapato na ajira katika mkoa huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Askofu Bagonza: CDF Mabeyo amepasua masikio yetu

Spread the loveMJADALA kuhusu safari ya mwisho ya maisha ya Hayati Rais...

Habari za Siasa

10 matatani kwa kutorosha madini ya bil 1.5

Spread the loveJeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Kikosi...

Habari za Siasa

Wagombea 127 wa udiwani kutoka vyama 18 kuchaguliwa kesho

Spread the loveWagombea udiwani 127 kutoka vyama 18 vya siasa wanatarajiwa kupigiwa...

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

error: Content is protected !!