Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CUF amtega Rais Magufuli
Habari za Siasa

Mbunge CUF amtega Rais Magufuli

Spread the love
MBUNGE wa Kilwa Kusini (CUF), Sulemani Bungala ameitaka serikali kuruhusu wavuvi wadogo wadogo kuendelea na shughuli zao. Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni leo Jumanne, Bungala alisema, ni jambo la kusikitisha kuona serikali inaruhusu viwanda vya nyavu vinatengeneza bidhaa hiyo yenye matundu madogo na kuziuza kwa wananchi na kisha serikali kukusanya kodi.

“Mimi sielewi serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Siielewi kabisa. Yaani mimi binafsi, jamni siielewi serikali ya Rais John Pombe Magufuli. Inaruhusu viwanda vya nyavu kutengeneza nyavu zenye matundu madogo; na kisha inapokea kodi ya viwanda hivyo, lakini baadaye inashughulika na wavuvi. Siwaelewi,” alieleza Bungala.

Alisema, “Serikali ya CCM chini ya Rais Maguli, inatoa leseni kwa wavuvi, lakini ghafla inawageuka wavuvi hao hao wenye leseni na kuwanyang’anya nyavu zao na kisha kuwaita wavuvi haramu.”

Mbunge huyo ambaye anafahamika kwa jina la utani la Bwege alisema, “namtaka rais wa wanyonge, awaruhusu wavuvi hawa wa Kilwa Kusini na maeneo mengie, watumie nyavu zao, ili mradi wana leseni ya uvuvi. Maana kama wanyonge, basi wanyonge wenyewe ni wavuvi.”

Bungala alitoa kauli hiyo wakati akichangia hotuba ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi na Maliasili. Bunge limepanga kwa siku mzima ya leo, kujadili ripoti ya kamati hiyo na ile ya Kilimo, Maji na Mazingira.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!