Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema atinga uraiani
Habari za Siasa

Mbunge Chadema atinga uraiani

Wabunge Ester Bulaya na Halima Mdee
Spread the love

HATIMAYE mbunge wa Bunda (Chadema), Ester Bulaya amepata dhamana baada ya kushikiliwa na Polisi kanda maalum ya Tarime na Rorya kwa amri ya Mkuu wa wilaya ya hiyo Glorious Luoga, anaandika Mwandishi Wetu.

Kabla ya kupata dhamana leo hii, wanachama wa Chadema kutoka maeneo mbalimbali mkoani Mara ikiwamo jimboni kwake, walifurika kituo cha polisi.

Kutokana na wingi wa wananchi hao wakiongozwa na Mbunge wa Tarime vijijini, John Heche, polisi wameonekana kuweka ulinzi mkali.

mwishoni mwa wiki, Bulaya alikamatwa na jeshi la Polisi akiwa katika Hotel ya Kifa Best Point Wilayani Tarime akidaiwa kujiandaa kutaka kufanya mkusanyiko kinyume cha sheria.

Kamanda wa polisi Tarime/Rorya Kamishina Msaidizi Mwandamizi Henry Mwaibambe alisema Bulaya hakutakiwa kushiriki katika mkutano wa Ester Matiko (Chadema), ambaye ni mbunge wa Tarime mjini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!