Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema aliyekamatwa, atoka ‘sero’
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Chadema aliyekamatwa, atoka ‘sero’

Spread the love

JESHI la Polisi wilayani Tarime limewaachia kwa dhamana, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko (Chadema) na Mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Sitta Tuma. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).

Matiko na Tuma walikamatwa jana tarehe 8 Agosti, 2018 na Jeshi la Polisi wakiwa kwenye mkutano wa kumnadi mgombea udiwani Chadema Kata ya Turwa.

Polisi waliuzuia mkutano huo kwa sababu ya Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi Tarime kuzuia mikutano ya chama hicho.

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Twitter amesema Matiko na Tuma wameachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuripoti tena polisi hapo kesho.

Vile vile, Polisi imewaachia kwa dhamana wanachama wa Chadema kumi na nane waliokamatwa jana katika mkutano huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!