Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Chadema aitaka Serikali kutoa taarifa ya masoko
Habari za Siasa

Mbunge Chadema aitaka Serikali kutoa taarifa ya masoko

Frank Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma
Spread the love

MBUNGE Tunduma, Frank Mwakajoka (Chadema) ameitaka serikali kutoa taarifa ya masoko kwa wafanyabiashara ya mahindi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mwakajoka alitoa kauli hiyo Bungeni alipokuwa akiuliza swali la nyongeza, amesema kuwa serikali imekuwa na tabia ya kuwazuia wafanyabiashara wa nafaka nje kwa kisingizio cha njaa. 

Aidha Mwakajoka ametaka kujua kama serikali ina mpango wa kuwatangazia masoko kwa kuwa bunge halionyeshwi moja kwa moja kutokana na hilo wafanyabiashara hawawezi kujua masoko yalipo.

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stella Manyanya amesema kuwa kwa sasa kuna chakula cha kutosha nchini hivyo ruksa kuuza chakula kwenye masoko ya nje.

Aidha Mhandisi Manyanya amesema kuwa wafanyabiashara wanaotafuta masoko wapitie wizara husika kwa kutumia simu au njia ya mitandao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!