Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM aibana Serikali ubovu wa mashine za EFD’s
Habari za Siasa

Mbunge CCM aibana Serikali ubovu wa mashine za EFD’s

Spread the love

SERIKALI imetakiwa kutoa taarifa ya uhakika juu ya sakata la kutofanyakazi kwa Mashine za Kieletroniki (EFD’s) huku ikidaiwa kuwa kitendo cha mashine hizo kutofanya kazi na serikali kukaa kimya ni hujuma kwa uchumi wa nchi. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Sakata hilo lilibuliwa jana Bungeni baada ya Mbunge wa Sumve (CCM), Richard Ndasa, kuitaka serikali kutoa ufafanuzi kuhusu sakata hilo alilolifananisha na hujuma kwa uchumi wa nchi.

Ndasa amesema kuwa tangu Juni 11 mwaka huu hadi sasa, mashine hizo hazifanyi kazi na mnunuzi yeyote wa bidhaaa hawezi kupatiwa risiti za kieletroniki, hivyo mapato ya kodi stahiki ya serikali yanapotea.

Mbunge huyo ameomba maelezo hayo ya serikali leo baada ya kuomba mwngozo kwa Mwenyekii wa Bunge, Mussa Zungu, wakati ambao Bunge likiwa linaendelea na mjadala wa hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Amesema kuwa tangu tarehe aliyoitaja mtu yoyote akienda kununua kitu hawezi kupewa risiti za kieletroniki na kueleza kuwa kutokana na hali hiyo ni hakika kuwa mapato mengi ya serikali yatapotea.

“Ningependa kujua sasa, kwa sababu wiki ya kwanza, ya pili na ya tatu mashine hizi hazifanyi kazi, je, serikali inasemaje kuhusu tatizo hili ambalo ni janga la kitaifa?,” amehoji.

Ndasa amesema tatizo hilo linawezekana likawa ni hujuma kutoka kwa watu wasioitakia mema nchi.

Mara baada ya Ndasa kuomba ufafanuzi, huo Zungu alimtaka Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Ashantu Kijaji, kutoa kauli ya serikali Bungeni.

Akitoa kauli kuhusu sakata hilo, Dk. Ashantu ameeleza na kukiri kuwa ni kweli tatizo hilo lipo tangu Mei 11 mwaka huu, lakini lilishughulikiwa na kupatiwa ufumbuzi ndani ya wiki moja hata hivyo lilijirudia tena.

“Sasa hivi taasisi yetu ya E-Governament (Wakala wa Serikali Mtandao) kwa kushirikiana na kitengo cha ICT cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wanaendelea kulishughulikia kwa nguvu zote ili hali ijurudie kama kawaida,” amesema Dk. Ashantu.

Amesema serikali inafahamu changamoto za tatizo hilo na ndio maana wataalam bado wanaendelea kulishughulikia na matumaini yaliyopo litapatiwa ufumbuzi mapema iwezekanavyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!