Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbunge awakingia kifua wavamizi
Habari Mchanganyiko

Mbunge awakingia kifua wavamizi

Msitu wa Minyugye ulioppo wilaya ya Ikungi. Picha ndogo ni Elibariki Kingu, Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi
Spread the love

ELIBARIKI Kingu, Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi anatuhumiwa kuchochea kuongezeka kwa vitendo vya uvamizi katika msitu wa hifadhi wa Minyughe, wilayani Ikungi, anaandika Mwandishi wetu.

Mbunge huyo anadaiwa kuwalipia faini wananchi ambao wamekuwa wakikamatwa, kushtakiwa na kuhukumiwa mahakamani kwa makosa ya uvamizi wa msitu huo. Anadaiwa kutumia nafasi hiyo kama jukwaa la kisiasa la kumuongezea ushawishi kwa wananchi.

Taarifa hizi zinakuja wakati ripoti zikiwa zinaonesha kuwa zaidi ya wakazi 41 wa kijiji cha Mtavira, kata ya Makilawa, Wilaya ya Ikungi, mkoani Singida wamefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Ikungi kwa tuhuma za kuvamia msitu wa hifadhi ya Minyughe.

Michael Lyimo, Kaimu Meneja wa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) amesema, “Tuafanya juhudi kubwa lakini bado matokeo siyo mazuri sana kwani wananchi waliohukumiwa kwa uvamizi wanalipiwa adhabu ya faini na Mbunge wao. Kama wangelipa wenyewe wangeona umuhimu wa kutovamia msitu wa hifadhi.”

Lyimo amedai kuwa wanasiasa wamekuwa wakiutumia msitu huo kujipatia umaarufu wa kisiasa na kusaka kura kwa kuwashawishi wananchi kuwa waendelee kuishi ndani ya msitu huku wanasiasa wengine wakiahidi kuufanya msitu huo wa hifadhi kuwa eneo la makazi iwapo watachaguliwa.

Mpaka sasa, jumla ya kaya 76 zilizokuwa zikiishi katika nyumba zilizokuwa ndani ya hifadhi zimehamishwa kwa nguvu na nyumba hizo kuvunjwa.

“Nawasihi wanasiasa watafute namna nyingine ya kuomba kura na kutafuta umaarufu wa kisiasa kwasababu uhifadhi wa mazingira una faida nyingi hata kwa kizazi kijacho, hivyo historia itakuja kuwahukumu waharibifu wa mazingira,” amefafanua Lyimo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!