Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge aliyetishia kuhamia CCM, ahamia kweli
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge aliyetishia kuhamia CCM, ahamia kweli

Spread the love

MBUNGE wa Serengeti (Chadema), Marwa Chacha amejiuzulu uanachama wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza leo Septemba 27, 2018 Chacha amesema amechukua uamuzi huo kumuunga mkono mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli.

Amesema wakati akigombea ubunge aliahidi kuwaletea maendeleo wananchi wake lakini dhamira yake haijafanikiwa kutoka na vikwazo anavyokumbana navyo ndani ya Chadema.

Chacha amewataka wakazi wa Serengeti kumchagua mtu atakayeweza kushirikiana nao pamoja ili kuleta maendeleo kupitia CCM.

Mbunge huyo alikutana na wakati mgumu wakati wa ziara ya Rais Magufuli mkoani Mara ya kuzomewa na wananchi alipobanwa na maswali.

Baada ya kuzomewa Chacha alipopata nafasi kuzungumza alisema, wanamzomea kwa sababu yeye siye CCM lakini ipo siku naye atakuwa CCM.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!