Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge akataliwa kusajili shule
Habari za Siasa

Mbunge akataliwa kusajili shule

Prof. Joyce Ndalichako, Waziri wa Elimu
Spread the love

MBUNGE wa jimbo la Itilima, Njalu Silanga (CCM) amekataliwa kupewa usajili wa shule  ya msingi Njalu iliyopo wilayani Itilima Mkoani Simiyu kwa sababu ya kutokidhi vigezo, anaandika Mwandishi wetu.

Usajili wa shule hiyo iliyojengwa na wananchi kwa kushirikiana na Mbunge Njalu Silanga wa jimbo la Itilima (CCM) umekataliwa na Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako.

Profesa Ndalichako amesema shule hiyo haijakidhi vigezo vya usajili hivyo amekataa ombi la mbunge huyo kuisajili na kuagiza upungufu uliopo urekebishwe kwanza kabla ya wizara kuisajili shule hiyo ya umma.

Miongoni mwa upungufu huo ni kuwa na vyumba vitano pekee vya madarasa kati ya vinane vinavyohitajika.

Mengine ni matundu ya vyoo, ambayo kati ya 10 yanayohitajika, yapo matano pekee, huku ikiwa na chumba kimoja cha ofisi ya walimu.

Hata hivyo, Profesa Ndalichako amesema wizara itatoa mifuko 100 ya saruji kusaidia kuondoa upungufu uliopo.

“Tumeona kuna upungufu hatutaweza kutoa kibali cha kuisajili, badala yake mkamilishe yanayohitajika kwa utaratibu wa kisheria wa kufungua shule. Niwahakikishie kuwa, Wizara ya Elimu hatuna urasimu ni lazima tuwe makini kwa kusimamia vigezo hivyo,” amesema Profesa Ndalichako.

Amesema licha ya kuwapo kwa mahitaji ya shule katika eneo hilo ambalo lina wanafunzi wapatao 633, ni lazima kuzingatia vigezo ambavyo vitakaguliwa na wataalamu kutoka idara ya udhibiti ubora wa elimu na ofisi ya ofisa elimu wilaya.

Silanga alimwomba Waziri Ndalichako kuwapatia usajili wakati wakiendelea kushughulikia upungufu uliojitokeza kwa kipindi cha muda mfupi kabla ya shule kufunguliwa Januari 8 mwakani ombi ambalo hata hivyo, lilikataliwa.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!