FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amefika leo tarehe 31 Januari, 2019 kwenye mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuhudhuria kesi inayomkabili yeye na viongozi waandamizi wa chama hicho akionekana mwenye afya njema. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Mbowe na viongozi waandamizi wengine wanane wa chama hicho wanashtakiwa kwa kufanya mkusanyiko na maandamano yanayodaiwa kuwa siyo halili.
Tarehe 17 Januari 2019 Mbowe alishindwa kuhudhuria mahakamani hapo kwa kilichoelezwa na upande wa mashataka kuwa anaumwa.
Mbowe na Ester Matiko Mbunge wa Tarime Mjini ambao wamefutiwa zao dhamana tangu Mwezi Novemba mwaka jana kwa kilichotajwa kuwa amekwenda kinyume na mashaart ya dhamana.
Viongozi wengine wanaoshitakiwa kwenye kesi hiyo ni pamoja na Vincent Mashinji, Katibu Mkuu wa Chama hicho, Salum Mwalimu Naibu Katibu Mkuu Z’bar, John Mnyika, Mbunge Naibu katibu Mkuu Bara, John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini, Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, Mch. Peter Msigwa Mbunge wa Iringa Mjini.
Leo mbele ya Hakimu Mfawidhi Kelvin Mhina ambaye amepokea kesi hiyo kwa aliyekuwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri ambaye ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Wakili wa serikali Wankyo Simon ameieleza mahakama kuwa kesi hiyo imefika kwa ajili ya kutajwa mpaka pale rufaa ya dhamana iliyoombwa na upande wa utetezi mahakama kuu itakaposikilizwa.
Baada ya maelezo hayo wakili wa upande wa utetezi, Profesa Abdallah Safari ameieleza mahakama hiyo kuwa rufaa itasikilizwa tarehe 18 Februari mwaka huu.
Hakimu mhina ameihalisha kesi hiyo na kuitaja tena tarehe 14 Februari mwaka huu.
Viongozi hao wanashtakiwa mahakamani hapo kwa makosa 13 pamoja na kula njama ya kufanya ghasia, kufanya maandamano kinyume cha sheria, kuhamasisha chuki, kufanya uchochezi na wanadaiwa kutenda makosa hayo terehe 1 na 16 Februari mwaka 2017.
https://www.youtube.com/watch?v=S9VOZ4NOC0g&feature=youtu.be
Leave a comment